Habari Za Un

Wanawake wajengewa uwezo wa tofauti ya matumizi ya lazima ni muhimu ili kujikwamua kiuchumi

Informações:

Synopsis

Mwaka 1995 huko Beijing, China kwenye mkutano wa nne wa kimataifa wa wanawake lilipitishwa Azimio la Beijing na Mpango wa Utekelezaji, ambalo pamoja na mambo mengine lililenga kusongesha haki za wanawake. Mwaka huu wa 2025 ikiwa ni miaka 30 baadaye, tathmini ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, inaonesha kuwa nchi zimesonga mbele katika usawa wa jinsia na uwezeshaji wanawake, kuanzia kuharamaisha ubaguzi kwenye ajira hadi mipango ya kuhimili tabianchi inayozingatia jinsia. Lakini bado kuna vikwazo vya kijamii, kiuchumi na kisiasa na ndio maana wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake mwaka huu wa 2025 kipaumbele ni kusongesha uwezeshaji, haki na usawa. Ni katika kumulika harakati hizo, Assumpta Massoi anakupeleka Singida nchini Tanzania kwenye maadhimisho yaliyoambatana na ujengeaji uwezo.