Gurudumu La Uchumi
- Author: Vários
- Narrator: Vários
- Publisher: Podcast
- Duration: 3:54:15
- More information
Informações:
Synopsis
Fahamu masuala kadha wa kadha kuhusu uchumi kama vile, namna ya kupambana na umaskini, mfumuko wa bei, kushamiri kwa matumizi ya dola na athari za kuyumba kwa uchumi wa dunia kwa nchi za Afrika. Mada hizi zinafanyiwa utafiti wa kina na zinazungumzwa kwa lugha rahisi inayoeleweka ili kukufanya uelewe na usichoke kusikiliza .
Episodes
-
Tatizo la uhaba wa dola ya Marekani kwenye nchi za Afrika Mashariki
22/09/2023 Duration: 09minKatika Makala ya Gurudumu la Uchumi juma hili, mtayarishaji wa makala haya amezungumza na Profesa Wetengere Kitojo, mtaalamu wa masuala ya uchumi akiwa Tanzania, ambapo wanaangazia kuhusu tatizo la uhaba wa dola ya Marekani kwenye nchi za Afrika Mashariki.
-
Biashara ya madini yaimarika nchini DRC
07/09/2023 Duration: 09minWiki hii tunaangazia huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambako kunaripotiwa ongezeko kubwa la uzalishaji wa madini ya shaba na kobalt katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Takwimu kutoka sekta ya madini, zinaonesha kuwa uzalishaji wa kobalt imeongezeka na kufikia zaidi ya Tani Laki moja, baada ya serikali kuwekeza asilimia 43 ya bajeti yake ya taifa kwenye sekta hiyo. Kwenye Makala haya, mwandishi wetu wa Lubumbashi Denise Maheho, amezungumza na watafiti wa madini na mashirika ya kiraia, katika eneo la Katanga.
-
Nguo za mitumba zapigwa marufuku nchini Uganda
01/09/2023 Duration: 09minSerikali ya Uganda imepiga marufuku uingizwaji na uuzwaji wa nguo kukuu maarufu kama mitumba nchini humo. Rais Yoweri Museveni anasema, hatua hiyo itasaidia kukusa viwanda vya ndani vya nguo na kuunda ajira hasa kwa vijana. Mwandishi wetu wa Kampala Kenneth Lukwago anatueleza zaidi.
-
MABADILIKO YA TABIA NCHI KWA UCHUMI
10/08/2023 Duration: 10minAthari za mabadiliko ya tabia nchi kuanzia mafuriko na ukame zimesababisha mamilioni ya raia kupoteza makazi yao, wengi wakitumbukia katika hali ya umasikini na hata kufa njaa, baadhi wakikosa huduma muhimlu ya afya, elimu huku tofauti kati ya walionacho na wasionacho ikiendelea kuongezeka, uchumi wa mataifa ukidorora. Kwa mujibu wau moja wa Mataifa mpaka kufikia mwaka 2030 watu wanaokadiriwa kufikia milioni 700 huenda wakawa wakuhamahama kutokana na ukame peke yake.Kuchukua hatua stahiki kukabili mabadiliko ya tabia nchi na athari zake ni jambo lisilohitaji mjadala wa muda mrefu ili kunusuru maisha ya raia pamoja na kufikia malengo endelevu ya umoja wa Mataifa.Haya yanajiri wakati huu joto likiendelea kuongezeka, nchi zikitumia fedha nyingi kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi badala ya kuwa zingeelekezwa katika kutatua changamoto za maendeleo na kiuchumi hasa kwenye nchi masikini.Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, inaangazia ni namna gani nchi zinazoendelea zinaweza kukabiliana na athari z