Synopsis
Jua Haki Zako ni makala yanayokuelimisha juu ya umuhimu wa kufahamu haki zako na sheria halali zilizomo kwenye jamii, mataifa na dunia kwa ujumla. Jua Haki Zako itakuelimisha juu ya masuala mbalimbali ya kisheria ndani ya Afrika Mashariki, Afrika na Duniani kwa ujumla.
Episodes
-
Kenya : Sanaa ya wanafunzi wa shule yakera serikali
21/04/2025 Duration: 09minMjadala makali bado unaendelea baada ya serikali kudaiwa kuzuia wanafunzi wa shule ya upili ya Butere kuwasilisha uchezo wao wa Echoas of War kwenye ngazi ya kitaifa kwenye mashindao ya kuingiza. Kisa na maana ni kwamba mchezo huo unaikosoa serikali na kwamba uliandikwa na mwanasiasa ambaye ni katibu mkuu wa zamani wa chama tawala cha UDA, Bwana Cleophas Malala. Kauli ya wanafunzi kupitia mchezo wa kuigiza wa "Echoes of Doom" imeibua maswali mazito kuhusu uhuru wa kujieleza, demokrasia na usalama wa taifa.Wanafunzi hawa walitumia jukwaa la sanaa kuelezea hali halisi ya jamii, lakini kile kilichoanza kama onyesho la kisanaa , limeibua hisia mseto baada ya madai kwamba serikali iliwazuia wanafunzi hao kuonyesha sana hiyo kwenye ngazi ya kitaifa. Skiza makala haya kufahamu mengi zaidi.
-
Haki ya maakazi bora kwa jamii zetu
07/04/2025 Duration: 10minKatika makala haya tunajadili haki ya raia kuwa maakazi bora ambapo maelfu ya wazee, walemavu, na wajane nchini Kenya wamekuwa wakikabiliwa na changamoto kubwa za makazi duni, hasa katika maeneo kame na mitaa duni. Hali hii imewalazimu wengi kuishi katika mazingira yasiyofaa, huku baadhi yao wakikosa makazi kabisa. Hata hivyo, kwa ushirikiano wa wahisani, mashirika ya kijamii, na serikali za kaunti, mpango wa kuwajengea makazi bora umeanzishwa katika kaunti mbalimbali, ukiwapa matumaini wapate hifadhi salama na yenye hadhi.Katika kijiji cha Naibor, Kaunti ya Laikipia, baadhi ya wazee tayari wameanza kunufaika na mpango huu. Skiza maka haya kufahamu mengi
-
Wazee na Wasiojiweza wafaidika na Mpango wa Makazi Bora Nchini Kenya
07/04/2025 Duration: 10minMaelfu ya wazee, walemavu, na wajane nchini Kenya wamekuwa wakikabiliwa na changamoto kubwa za makazi duni, hasa katika maeneo kame. Hali hii imewalazimu wengi kuishi katika mazingira yasiyofaa, huku baadhi yao wakikosa makazi kabisa. Hata hivyo, mpango wa kuwajengea makazi bora umeanzishwa katika kaunti mbalimbali, ukiwapa matumaini wapate hifadhi salama na yenye hadhi. Katika kijiji cha Naibor, Kaunti ya Laikipia, baadhi ya wazee tayari wameanza kunufaika na mpango huu.
-
Tamaduni na sheria zetu wapi Mipaka ?
31/03/2025 Duration: 09minKwenye makala haya tunajikita na kuzama kuangazia tafauti iliopo kati ya haki, sheria na dhuluma dhidi ya wanawake. Haya yote ni kutoka na familia moja nchini Kenya eneo la Narok, ambayo inalilia haki baada ya msichana wao kutetendwa vitendo vya kinyama kutokana tamaduni za jamii ya Kisii kumtaka amwange mchanga ndani ya kaburi la aliyekuwa bwana yake kinyume na matakwa yake.Skiza makala haya kufahamu mengi zaidi.