Synopsis
Makala ya Wimbi la Siasa inakupa fursa ya kufahamu masuala ya kisiasa yanayoendelea ndani na nje ya Bara la Afrika. Kwenye Makala haya utapata habari ambazo zinakugusa moja kwa moja wewe msikilizaji. Kila wakati usikose kusikiliza Makala ya Wimbi la Siasa
Episodes
-
Nini suluhu ya mzozo wa Mashariki mwa DRC ?
29/01/2025 Duration: 10minWiki hii mapigano makali yameshuhudiwa jijini Goma, kati ya wanajeshi wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa M 23 wanaoripotiwa kuungwa mkono na nchi ya Rwanda. Nini suluhu ya mzozo wa Mashariki mwa DRC ?
-
Rais Samia ateuliwa na cham chake kuwania urais mwaka 2025
22/01/2025 Duration: 10minRais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameteuliwa kwa kauli moja na wajumbe wa chama cha mapinduzi CCM kupeperusha bendera ya chama hicho wakati wa uchaguzi mkuu mwezi Oktoba. Tunachambua hatua hii.
-
Vita Mashariki mwa DRC vyawaathiri maelfu ya watu Masisi
15/01/2025 Duration: 10minTunaangazia kuendelea kwa vita Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kati ya jeshi la serikali FARDC wanaoshirikiana na wapiganaji wa Wazalendo dhidi ya waasi wa M 23 wanaoungwa mkono na Rwanda. Watu zaidi ya 100, 000 wameyakimbia makaazi yao katika wilaya ya Masisi tangu kuanza kwa mwaka 2025 kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.Nini suluhu ya mzozo huu ?
-
Tanzania: Mbowe na Lissu wakiweka CHADEMA njia panda
08/01/2025 Duration: 10minChama kikuu cha upinzani nchini Tanzania CHADEMA, kitawachagua vongozi wa ngazi ya juu wa chama hicho, Januari tarehe 21. Kibarua kigumu kipo kwenye ushindani wa nafasi ya Mwenyekiti.Freeman Mbowe ambaye amekuwa akiongoza chama hicho kwa zaidi ya miaka 20 na Makamu wake Tundu Lissu, ni miongoni mwa watia nia waliojitosa kupambania nafasi hiyo.Wawili hao wameendelea kutupiana maneno makali, na kuzua hofu kuhusu hatima ya chama hicho baada ya uchaguzi huo. Thomas Kibwana ni mchambuzi wa siasa za Tanzania, akiwa jijini Dar es salaam, anachambua kwa kina.