Synopsis
Makala inayojadili kwa kina masuala ya afya, tiba na kutambua magonjwa mbalimbali bila ya kusahau namna ya kukabiliana nayo. Watalaam walibobea kwenye sekta ya afya watakujuvya na kukuelimisha juu ya umuhimu wa kuwa na afya bora na si bora afya. Pia utawasikiliza kwa maneno yao watu ambao wameathirika na magonjwa mbalimbali na walikumbwa na nini hadi kufika hapo walipo.
Episodes
-
Ufanisi wa Tiba asili nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
07/04/2025 Duration: 10minWaganga wa tiba asilia wana mchango katika ulimwengu wa uzalishaji dawa
-
Ukosefu wa maji salama unavyozidisha hali ya kibinadaam barani Afrika
26/03/2025 Duration: 10minKuna idadi kubwa ya watu wanaoshindwa kupata maji salama kwa matumizi ya nyumbani ,hospitali na hata mashamba Uhaba wa maji unaorodheshwa kuwa sababu kubwa ya watu kukosa chakula, kujikimu katika nchi zinazoshuhudia migogoro.Katika nchi kama Sudan na DRC kuna ripoti za hospitali ,kambi za wakimbizi kukosa moja hivyo mashirika ya kimsaada yanapata changamoto kuwahudumia wakimbizi
-
Mpango wa lishe katika shule za umma nchini Kenya kupambana na utapiamlo
19/03/2025 Duration: 10minUkosefu wa lishe bora huathiri afya na elimu nchini Kenya Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la linalowahudumia Watoto (UNICEF) imeonesha kuwa takriban watoto milioni mbili nchini Kenya wanakabiliwa na matatizo yanayotokana na utapiamlo. Mipango ya lishe bora shuleni eneo la Nyanza na maghari mwa Kenya umeonekana kuwa suluhu huku wanafunzi wakipata vyakula vilivyo na virutubishi bora vinavyosaidia kuboresha kinga ya mwili,hivyo kuimarisha afya .
-
Haja ya huduma muhimu za wanawake waja wazito kupatikana kwa urahisi
11/03/2025 Duration: 10minWHO imetaja ukosefu wa huduma za kuokoa maisha wakati wa kujifungua huchangia vifo vingi vya wanawake waja wazito Huduma hizo za wanawake hata hivyo zina bei kubwa