Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

  • Author: Vários
  • Narrator: Vários
  • Publisher: Podcast
  • Duration: 8:02:40
  • More information

Informações:

Synopsis

Makala yanayochambua masuala na matukio mbalimbali yaliyotokea kwenye jamii kwa wiki nzima kwa kina, yanatoa fursa kwa msikilizaji kueleza hisia na mtazamo wake juu ya masuala yanayoendelea kutokea iwe ni katika uga wa uchumi na siasa duniani kote.

Episodes

  • Kiongozi wa Chama cha upinzani Tanzania Chadema ashikiliwa kwa uhaini, hali ya DRC

    12/04/2025 Duration: 20min

    Matukio ya wiki: kukamatwa kwa mwenyekiti wa chama cha upinzani cha Chadema nchini Tanzania, Tundu Lisu, maadhimisho ya miaka 31 ya mauaji ya kimbari ya nchini Rwanda mwaka 1994, mafuriko jijini Kinshasa huko DRC, hali ya sudan Kusini kutokana na kukamatwa na kuzuiwa nyumbani kwa makamu wa kwanza wa rais Riek Machar, uchaguzi wa Gabon, na pia mzozo wa kibiashara kati ya Marekani na mataifa mengine ulimwenguni ni miongoni mwa Habari kuu za dunia zilizojiri kwa juma hili.

  • Ziara ya rais wa Uganda nchini Sudan kusini, waasi wa M23 wajiondoa Walikale

    05/04/2025 Duration: 20min

    Miongoni mwa matukio makubwa ya juma hili ni pamoja na ziara ya rais wa Uganda Yoweri Museveni, iliyotangulizwa na ziara ya wajumbe wa Umoja wa Afrika, nchini Sudan Kusini baada ya makamu wa rais wa nchini hiyo kukamatwa na kuzuiwa nyumbani kwake, kule DRC waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda waripotiwa kujiondoa katika mji wa Walikale mokowani Kivu kaskazini mashariki mwa DRC, tunaangazia Kenya, Uganda, nchi za Afrika mashariki na magharibi pia kwengineko duniani 

  • kukamatwa kwa makamu wa kwanza wa rais Sudan Kusini, waasi wa M23 waalikwa Doha

    31/03/2025 Duration: 20min

    Ni juma ambalo limeshuhudia kukamatwa kwa makamu wa kwanza wa rais wa sudan Kusini Riek Machar na kuzuiwa nyumbani kwake, rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye wiki hii aliishutumu Rwanda kwa kupanga kuishambulia nchi yake, waasi wa M23 kukutana na Kiongozi wa Qatar kule Doha,afisa wa polisi ya Kenya kule Haiti kutoweka, utawala wa kijeshi kule Niger kuzindua kipindi cha mpito cha miaka mitano, pia mashambulio ya Israeli kule Lebanon na mkutano wa Ulaya kuhusu Ukraine

  • Rais wa DRC Tshisekedi akutana na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame, vita nchini Sudan

    22/03/2025 Duration: 20min

    Yaliyomo ni pamoja na Mkutano wa ana kwa ana kati ya rais wa DRC Felix Tshisekedi na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame mjini Doha Qatar, mapigano kule Sudan Kusini kati ya wanajeshi wa serikali na wapiganaji wa white Army waliotiifu kwa makamu wa kwanza wa rais Riek Machar, Niger kujivua uanachama wa franchophonie, mashambulio ya Israeli kule Gaza, sintofahamu ya sitisho la mapigano kwa muda mfupi kati ya Urusi na Ukraine ni miongoni mwa habari kuu za dunia zilizojiri kwa juma hili.

page 2 from 2