Siha Njema

Afueni kwa wanawake wanaokatwa matiti yao kutokana na saratani

Informações:

Synopsis

Kila mwezi wa Oktoba, ulimwengu huadhimisha Mwezi wa Uhamasishaji wa Saratani ya Matiti, lengo kuu likiwa kuhamasisha vipimo vya mapema ili kupunguza hatari ya ugonjwa huu na kutafuta msaada wa kifedha kwa ajili ya utafiti kuhusu saratani ya matiti. Inakadiriwa kuwa, wagonjwa wapya zaidi ya milioni 2.3 wa saratani ya matiti hugunduliwa kila mwaka, kulingana na takwimu za Shirika la Afya Duniani. Wengi wa wanawake waliopatwa na saratani hii walilalzimika kukatawa titi moja au yote mawili ili kuokoa maisha yao,  na hivyo kupoteza kiungo muhimu cha mwili.