Gurudumu La Uchumi

Afrika na jitihada za kutaka kuwa katika meza ya majadiliano ya kidunia na sio mualikwa

Informações:

Synopsis

Msikilizaji wakati wa kongamano la kimataifa la wakurugenzi wakuu wa kampuni mbalimbali duniani waliokutana nchini Rwanda, maswali kadhaa yaliibuliwa, kubwa lilikuwa ni je bara la Afrika linapaswa kuwa katika meza ya maamuzi au kwenye orodha, na ikiwa huu ni muda muafaka wa kutoa mustakabali wake. Ni maswali magumu ambayo hata hivyo viongozi wa Afrika walioshiriki, wanakubaliana kuwa bara hili lina rasilimali zakutosha kubadili uelekeo wake na maendeleo kwa raia, lakini pia halipaswi kuwa linaomba kwa viongozi wa magharibi kuwa katika meza ya majadiliano kuhusu mustakabali wa uchumi na maendeleo ya dunia. Suala la mabadiliko ya tabia nchi na utekelezaji wa mkataba wa biashara huria wa bara hili, maarufu kama AfCFTA, liliibuka, ambapo licha ya utiwaji saini itifaki yake, bado kuna vikwazo vya kufanya biashara baina ya nchi za Afrika.